Mikopo
hutolewa kwa waombaji wa elimu ya juu waliotimiza sifa na vigezo kama
vinavyoainishwa na kifungu cha 20 cha Sheria Namba 3/2011 na kifungu cha 3 cha
Kanuni za Bodi.
Kulingana na
tafsiri iliyotolewa na Sheria ya Bodi, elimu ya juu ni ngazi ya elimu
inayoanzia Shahada ya Kwanza (Bachelor/First Degree) au ngazi
nyengine ya mafunzo inayolingana na shahada ya kwanza na kuendelea.
Elimu ya juu
hutolewa na vyuo vikuu na vyuo vyengine vya elimu ya juu ndani na nje ya nchi
vinavyotambuliwa na mamlaka husika nchini zikiwemo Kamisheni ya Vyuo Vikuu (Tanzania
Commission for Universities – TCU) na Baraza la Mafunzo ya Ufundi (The
National Council for Technical Education - NACTE).
Sheria Namba 3 ya 2011 inatoa mamlaka
kwa BMEJZ ya kuongoza na kusimamia mchakato wa utoaji mikopo kwa waombaji kulingana na mahitaji na uwezo uliopo kwa
wakati husika. Mamlaka ya Utoaji Mikopo ya BMEJZ ni pamoja na:
a)
Kuamua vipengele vya mafao ya mkopo atakavyopatiwa muombaji;
b)
Kuweka vigezo na sifa za msingi kwa muombaji
wa mkopo;
c)
Kuweka masharti maalum ya utoaji wa mikopo;
d)
Kuamua idadi ya waombaji watakaopata mkopo
kwa kila mwaka; na
e)
Kusimamia fani za masomo kulingana na vipaumbele
vya SMZ wakati wa utoaji wa mikopo.
Kifungu cha 19(1) cha Sheria ya Bodi kinaitaka BMEJZ kutoa mkopo kwa kila muombaji, aliyetimiza vigezo na sifa za msingi za kupatiwa mkopo zilizowekwa na BMEJZ, ili aweze kulipa gharama zote au sehemu ya gharama za elimu ya juu kwa kipindi chote atachokuwa masomoni.
Taarifa zilizoingizwa kwenye mfumo wa
kompyuta hutumika kutoa mapendekezo ya awali ya uteuzi wa waombaji wa mikopo
ambao wametimiza sifa za msingi za uteuzi kwa mwaka husika. Orodha ya waombaji kwa kila ngazi ya masomo
inayoombwa kulingana na uzito wa sifa za kila muombaji na fani iliyoombwa
hutayarishwa kwa ajili ya uteuzi.
Vigezo vinavyotumika kutoa mapendekezo
ya awali ya uteuzi wa waombaji watakaopatiwa mikopo unafuata utaratibu
uliowekwa na vifungu vya 19 na 20 vya Sheria Namba 3/2011 ya BMEJZ na
kufafanuliwa na vifungu vya 3 hadi 5 vya Kanuni za BMEJZ. Kwa ujumla vigezo
vinavyotumika kutoa mapendekezo ya uteuzi ni kama vifuatavyo:
·
Alama za ufaulu za waombaji.
·
Kuwepo kwa ithibati ya mwanafunzi kukubaliwa
kujiunga na chuo husika kabla ya uteuzi.
·
Fani inayoombwa kulingana na vipaumbele vya
SMZ.
·
Umri wa muombaji.
·
Uwiano wa idadi ya waombaji katika fani
mbalimbali.
·
Uwiano wa idadi ya waombaji wanaume na
wanawake wanaopendekezwa kupatiwa mikopo.
·
Uwezo wa fedha wa BMEJZ kutoa mikopo kwa
waombaji katika mwaka husika.
·
Uwepo wa waombaji waliopatiwa mikopo kutoka
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ya Jamhuri ya Muungano au Taasisi
na Asasi nyengine zinazotoa udhamini wa masomo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
Kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha Sheria Namba
3/2011 na kifungu cha 8 cha Kanuni za BMEJZ, mapendekezo ya uteuzi wa majina ya
waombaji wa mikopo yanatakiwa kuwasilishwa kwenye Kamati ya Elimu ya Juu inayoundwa na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa BMEJZ. Kazi ya Kamati ya Elimu ya
Juu ni kuhakiki, kujadili na kupitisha majina ya waombaji walioteuliwa kupatiwa
mikopo katika mwaka husika kwa kuzingatia vigezo vilivyotajwa hapo juu au
vyenginevyo kwa kadiri Kamati ya Elimu ya Juu itakavyoona inafaa kwa wakati
husika.
Hata hivyo, Kamati ya Elimu ya Juu imekasimu madaraka yake kwa Kamati ya Uteuzi ambayo uwepo wake
umetimiza matakwa ya kisheria kama ilivyotajwa katika kifungu cha 14(5) cha
Sheria ya BMEJZ. Kamati ya Uteuzi inaundwa na wajumbe watano wasiokuwa Wajumbe
wa Bodi ya Wakurugenzi ya BMEJZ. Wajumbe wa Kamati ya Uteuzi wanateuliwa na
Mhe. Waziri anayesimamia shughuli za Elimu.
Wajumbe hao watatoka:
·
Tume ya Mipango ya SMZ.
·
Wizara inayosimamia Elimu.
·
Wizara inayosimamia Utumishi wa Umma.
·
Sekta binafsi.
·
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (BMEJZ),
ambayo itawakilishwa na Meneja Mikopo atakayekuwa pia Katibu wa Kamati ya
Uteuzi.
Baada ya kumaliza kazi ya uteuzi wa
waombaji wa mikopo ya elimu ya juu, Mwenyekiti ya kamati ya Uteuzi atakabidhi
taarifa ya uteuzi’ pamoja na orodha za majina ya waombaji wanaopendekezwa
kupatiwa mikopo, kwa mwenyekiti wa Kamati ya Elimu ya Juu ambaye ataiwakilisha
katika Kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa BMEJZ kwa ajili ya kuridhiwa na kutoa idhini
ya kutangazwa kwa waombaji wote waliopatiwa mikopo.
Majina ya waombaji walioteuliwa kupatiwa mikopo hutangazwa kupitia tovuti ya BMEJZ (www.zhelb.go.tz), tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo wa Amali (www.moez.go.tz) au njia nyengine yoyote ambayo BMEJZ itaona inafaa na inayoweza kuwafikia watu wengi zaidi kwa urahisi.
Hakuna idadi maalum iliyowekwa ya
waombaji wanaoteuliwa kupatiwa mikopo kwa mwaka husika katika ngazi mbalimbali
za masomo. Idadi ya wanaoteuliwa inategemea upatikanaji wa fedha za kutosha
kukidhi mahitaji ya idadi kubwa ya waombaji wapya wa mikopo na idadi ya
wanafunzi wanaoendelea na masomo yao vyuoni kupitia mikopo wanayopatiwa na BMEJZ.
Wakati wa uteuzi kipaumbele hutolewa kwa
waombaji wanaotoka kwenye familia zenye kipato kidogo; wanawake na walemavu au
wazazi wa muombaji wote ni walemavu au wenye maradhi ya kudumu na kuthibitishwa
na daktari anayetambulika kuhusiana na kutokumudu kwao kujiingizia kipato cha
kuweza kumlipia gharama za masomo mtoto wao.
Hivyo waombaji wenye uwezo wa kujilipia
gharama za masomo au wanaotoka kwenye familia zenye uwezo wa kulipa gharama za
masomo wanashauriwa kutokuomba mikopo kutoka BMEJZ ili kutoa nafasi kwa
waombaji wasiojiweza kutumia nafasi chache za mikopo zilizopo.
Sifa za waombaji wa mikopo ambao maombi
yao yanaweza kuzingatiwa wakati wa uteuzi zimetajwa kwenye kifungu cha 20
zikiwemo:
a) Muombaji
awe Mzanzibari
b) Awe
ameomba mkopo kwa kujaza Fomu Nambari 1
au kupitia njia nyengine yoyote ile ambayo BMEJZ itaona inafaa. Maombi yawe
yamewasilishwa ndani ya muda maalum uliowekwa na BMEJZ unaoanzia Mei 2 hadi Julai 31 ya kila mwaka.
c) Awe
amepata udahili kwenye chuo cha elimu ya juu kinachotambuliwa na mamlaka husika
nchini.
d) Awe
amepata alama nzuri za ufaulu.
i.
Muombaji wa shahada ya kwanza (Bachelor/First
Degree) aliyehitimu kidato cha sita anapaswa awe amefaulu angalau
masomo mawili ya mlinganisho (Principal subjects) kwa alama za
ufaulu zinazoanzia alama (points) 4.0.
ii. Muombaji
wa shahada ya kwanza aliyehitimu stashahada ya kawaida (Ordinary Diploma) anatakiwa
awe na ufaulu unaoanzia alama (GPA) 3.0 au B. Wahitimu wa “Full Technician Certificate
(FTC)” wawe na ufaulu unaoanzia alama C.
iii. Muombaji
wa shahada ya uzamili (Master/Second Degree) katika masomo
ya sanaa au sayansi jamii awe amehitimu shahada ya kwanza na kupata alama za
ufaulu kuanzia daraja la pili la juu (upper second class). Waombaji wa shahada
ya uzamili katika masomo ya sayansi, ufundi, tiba, uchumi, mipango na biashara
wawe na alama za ufaulu za kuanzia daraja la pili la chini (lower second class). Wahitimu
wa stashahada ya uzamili(Postgraduate Diploma) wanapaswa kupata
alama za ufaulu kuanzia daraja la pili la chini (lower second class)
iv. Muombaji
wa shahada ya uzamivu (Doctor of Philosophy - PhD) awe
amehitimu shahada ya uzamili na kupata alama za kuanzia daraja la pili la juu
kwa waombaji wa masomo ya sanaa na sayansi jamii. Waombaji wa shahada ya
uzamivu katika masomo ya sayansi, ufundi, udaktari na uchumi, mipango na
takwimu wapate alama za ufaulu kuanzia daraja la pili la chini.
v. Waombaji
wanaoendelea na masomo vyuoni pia wanaweza kuomba kwa kuzingatia sifa za kitaaluma
zilizotajwa hapo juu [d(i) –(iv)]. Aidha muombaji awe amefaulu mitihani yake ya
chuo kwa kiwango kitakachomwezesha kuendelea na masomo kwa mwaka unaofuatia
katika ngazi ya masomo anayoombea mkopo.
e) Awe
ameomba fani inayolingana na vipaumbele vya SMZ katika mwaka husika.
f) Asiwe
na mkopo au udhamini wa masomo kutoka taasisi nyengine.
g) Muombaji
wa shahada ya kwanza asizidi umri wa miaka 35 wakati wa kuanza masomo na muombaji
wa shahada ya uzamili asizidi miaka 40. Ukomo wa umri wa muombaji wa shahada ya
uzamivu ni miaka 45 wakati wa kuanza masomo.
h) Muombaji
aliyeajiriwa kwenye utumishi wa umma awasilishe barua ya ruhusa kutoka kwa
mwajiri wake.
i) Muombaji
anayedaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar awe ameshaanza kulipa
deni lake kwa angalau asilimia 25 ya deni lote bila ya kusita kwa malipo ya
deni ya kila mwezi.
j) Muombaji
aliyesoma kwa mkopo kutoka BMEJZ awe ameshafanya kazi kwa angalau miaka miwili
baada ya kuhitimu masomo yake ya awali kabla ya kuomba mkopo mwengine kutoka
BMEJZ.
Angalizo:
·
Waombaji wanaotumia sifa za masomo ya kidato
cha nne kuomba udahili katika vyuo vikuu vya ndani au nje ya nchi ili kujiunga
na masomo ya Shahada ya Kwanza, maombi yao ya mkopo hayatozingatiwa. Mfumo wa
elimu wa Tanzania unaotumika kwa wakati huu unatambua sifa ya msingi kwa
wahitimu wa elimu ya sekondari wanaodahiliwa kwa masomo ya Shahada ya Kwanza au
ngazi inayolingana nayo katika vyuo vikuu na vyuo vyengine vya elimu ya juu ni
kuhitimu masomo ya kidato cha sita.
Tume ya Mipango ya SMZ imetoa taarifa
kuhusu utafiti uliofanywa juu ya hali ya utumishi nchini ambayo imeonesha uwepo
wa mahitaji makubwa ya wataalamu. Taarifa hiyo imeibua maeneo ya Vipaumbele vya
SMZ juu ya mahitaji ya wataalamu na imeagizwa kuwa taarifa hiyo itumike kama
kigezo muhimu kwa utoaji wa mafunzo ya elimu ya juu nchini ili kufikia
utekelezaji wa mipango na maendeleo ya rasilimali watu iliyo bora na itakayowaandaa
watu wenye ujuzi sahihi, taaluma, tabia na silka zenye tija zinazoendana na
mabadiliko ya mfumo wa ushindani wa soko la ajira na kufikia viwango vya juu
vya uzalishaji na utoaji huduma.
Ili kurahisisha utekelezaji wa
Vipaumbele vya SMZ katika utoaji wa mafunzo ya elimu ya juu kuanzia mwaka wa
masomo 2016/17 hadi 2019/20, Tume ya Mipango imevigawa vipaumbele hivyo katika
madaraja matatu tofauti kulingana na umuhimu wa kila kada kama inavyoonekana
katika jedwali la hapo chini.
Hivyo, kwa mwaka huu wa masomo, BMEJZ
itazingatia kikamilifu taarifa ya fani za vipaumbele ya Tume ya Mipango wakati
wa upokeaji wa maombi ya mikopo na uteuzi wa waombaji katika mwaka wa masomo
2017/18.
SEKTA |
FANI NA KIWANGO CHA KIPAUMBELE |
||
DARAJA LA KWANZA |
DARAJA LA PILI |
DARAJA LA TATU |
|
EDUCATION |
Science and Mathematics |
Curriculum Development |
Learning Materials Development |
|
Technical Vocational Training |
School science Laboratory Management |
|
|
Early Primary Education |
IT with Education in Science Subjects/Mathematics |
|
|
Geography and English language |
|
|
|
Geography and History |
|
|
|
History and English |
|
|
HEALTH |
Anaesthesiology |
Cardiology |
Biochemistry |
|
Dentistry |
Dermatology |
Chemistry |
|
Gastroenterology |
Endocrinology |
ENT |
|
Haematology |
General Surgeon |
General Medicine |
|
Medical imaging |
Medical Emergency |
Infectious diseases |
|
Neurosurgery |
Oncology |
Microbiology |
|
Obstetrics and Gynaecology |
Paediatric surgery |
Nephrology |
|
Opthalmology |
Physiotherapy |
Pharmacology |
|
Orthopaedic |
Psychiatry |
Pharmacy |
|
Pathology |
Neurology |
Plastic surgery |
|
Radiology |
Nursing and Midwifery |
Rheumatology, Allergy and Immunology |
|
Urology |
|
Virology |
LAND AND ENERGY |
Cartography |
Architect |
Environment Health Surveying |
|
Land Management |
Mining/Metallurgy Engineering |
|
|
Land Surveying |
Quantity Surveying |
|
|
Urban Planning |
Radiation Protection |
|
|
|
Renewable Energy and Atomic Energy |
|
PETROLEUM AND GAS |
Geology |
|
Petroleum Law |
|
Petroleum Chemistry |
|
|
|
Petroleum Engineering |
|
|
|
Geophysics |
|
|
|
Petroleum Economics |
|
|
|
Environmental Engineering (Oil and Gas) |
|
|
INDUSTRIES |
Biological/Chemical Laboratories Technicians |
|
|
|
Chemical Engineering |
|
|
|
Industrial Engineering (Production, Quality
Assurance, Product Design) |
|
|
|
Soil Expertise |
|
|
|
Water Engineering |
|
|
|
Water management |
|
|
TRADE |
Trade Economics |
International Business |
Trade Administration |
TOURISM |
Tourism Marketing |
Language Professions |
|
|
Cultural heritage and Conservation |
Tourism Management |
|
|
Hospitality |
|
|
|
Tourism Planning |
|
|
AGRICULTURE |
Aquaculture |
Agro Forests |
Agriculture Planning |
|
Irrigation Engineering |
Animal breading |
Agronomy |
|
Plant Breeding |
Animal Nutrition |
Animal Husbandry |
|
Plant Pathology |
Biotechnology |
Fisheries Science |
|
Soil science Disciplines |
Entomology |
Marine Science |
|
|
Food and nutrition |
Seed Technology |
|
|
Horticulture |
|
|
|
Microbiology |
|
|
|
Natural resources management |
|
|
|
Veterinary |
|
FINANCE |
Financial Market and Investment |
Insurance |
Banking and Business Administration |
|
Financial Management |
Procurement |
Tax Management |
|
Programme Analysis |
Risk and
Damage Evaluation |
|
TRANSPORT AND COMMUNICATION |
Computer Science and Engineering |
Port and Shipping Management |
|
|
Information, Communication Technology (ICT) |
Road Economists |
|
|
Telecommunication Engineering |
Pilot and Aircraft Engineering |
|
ENVIRONMENT |
Natural Resources Management |
Environment Impact Assessment |
|
|
|
Environment Planning and Management |
|
|
|
Waste Management |
|
ECONOMICS AND DEVELOPMENT PLANNING |
Monitoring and Evaluation |
Building Economics |
|
|
Specialized Economics (Educational health,
development etc). |
Entrepreneurship |
|
|
Statistics |
Human Resource Management, Planning and
Development |
|
|
|
International Development Policy and
Negotiation |
|
|
|
Local Government |
|
OTHER PROFESSIONAL |
|
|
Mass Communication |
|
|
|
International Relations |
Mafao ya mkopo ambayo BMEJZ inaweza
kutoa kwa muombaji yameanishiwa kwenye Kifungu cha 19(2) cha Sheria Namba 3/2011.
BMEJZ inaweza kutoa kwa ukamilifu au sehemu ya mafao ya mkopo yaliyoainishwa
ambayo yanajumuisha:
a)
Ada ya masomo
b)
Ada ya mitihani
c)
Posho la chakula na makazi
d)
Gharama za vitabu na vifaa vyenginevyo vya
kujifunzia
e)
Nauli (inayoweza kulipwa ama mwanzo na mwisho
wa kila mwaka wa masomo kwa wanafunzi wa vyuo vya ndani; au kulipwa mwanzo
wakati muombaji anakwenda chuoni kuanza masomo na baada ya kuhitimu masomo ya
mwaka husika kwa vyuo vya nje.)
f)
Posho la utafiti na/au kazi za vitendo
g)
Gharama kwa ajili ya mahitaji maalum ya
vitivo
h) Bima
ya afya
Hata hivyo, Bodi imepewa mamlaka ya
kisheria ya kuamua vipengele vya mafao ya mkopo atakavyopatiwa mwanafunzi
husika na vipengele vitavyobakia vichangiwe na mwanafunzi mwenyewe, mzazi au
mlezi wa mwanafunzi husika.
a)
Kila muombaji atakayeteuliwa kupata mkopo awe
tayari kujaza mkataba wa mkopo (Fomu Nambari 2) unaotolewa na BMEJZ
na kukamilisha taarifa zote pamoja na kufuata masharti yote yaliyoainishwa
kwenye mkataba. Mkataba huu unapaswa kujazwa mwanzo wa mwaka wa masomo kwa
wanafunzi wapya na kurejea kujaza mkataba mpya kila mwanzo wa mwaka mpya wa
masomo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo kwenye ngazi ya masomo
waliyokubaliwa kupatiwa mkopo na BMEJZ.
b)
Malipo ya ada ya masomo, ada ya mitihani na
gharama nyengine zinazopaswa kulipwa moja kwa moja kwa chuo zitalipwa kupitia
akaunti ya chuo husika au njia nyengine ambayo BMEJZ itaona inafaa. Mtiririko
wa malipo ya ada ya masomo utalingana na muda wa masomo wa ngazi husika kama
utakavyoelezwa kwenye barua ya udahili.
c)
Posho zinazopaswa kulipwa moja kwa moja kwa
mwanafunzi, BMEJZ italipa kupitia akaunti itakayofunguliwa na mwanafunzi kwa
maelekezo ya BMEJZ au njia nyengine ambayo BMEJZ itakayoona inafaa. Malipo ya
posho yatalipwa kulingana na vigezo na uwezo wa Bodi. Kwa wanafunzi wa vyuo vya
nje, malipo ya posho yatafanyika kulingana na kiwango cha ubadilishaji fedha za
kigeni kilichotumika wakati wa kupitishwa kwa bajeti.
d)
Malipo ya mkopo yatatolewa kwa utaratibu wa
awamu au mkupuo kulingana na mfumo wa masomo katika Chuo husika au BMEJZ
itakavyoona inafaa kulingana na uwezo wake.
e)
Kiwango cha mkopo utakaotolewa kitakuwa na
ukomo wa mwisho wa malipo (ceiling) wa gharama za masomo
kwenye ngazi husika katika mwaka husika wa masomo. Mwanafunzi husika
atawajibika kujilipia gharama za ziada. Ukomo wa mwisho wa malipo kwa mwaka wa masomo kwa wakopaji wa
shahada ya kwanza ni shilingi 6,000,000/=; wakopaji wa shahada za uzamili shilingi
8,000,000/= na shahada za uzamivu ni shilingi 10,000,000/=.
f)
Wakopaji waliodahiliwa kwenye fani zinazosomeshwa
na vyuo vya ndani ya nchi kwa kushirikiana na vyuo vya nje ya nchi ambapo ada
ya masomo hutozwa kwa shilingi ya Tanzania kwa ajili ya chuo cha ndani na fedha
za kigeni kwa ajili ya chuo cha nje na kulipwa katika akaunti tofauti, BMEJZ
italipa ada inayotozwa kwa shilingi za Kitanzania pekee. Sehemu ya ada
inayotozwa kwa fedha za kigeni italipwa na mwanafunzi husika.
g)
Wakopaji waliojiunga/wanaojiunga na vyuo vya
nje kusoma fani adimu na zilizo kwenye vipaumbele vya SMZ watapatiwa aina moja
ya mafao ya mkopo kulingana na chaguo lake au kwa njia yoyote ile ambayo BMEJZ itaona
inafaa. Utaratibu huu umewekwa ili kuiwezesha BMEJZ kutoa mikopo inayorejesheka
na kuongeza idadi ya waombaji wanaopatiwa mikopo.
h) Muombaji
atakayerejea mwaka wa masomo katika ngazi husika, atapatiwa ruhusa ya kuendelea
kupatiwa mkopo kwa mwaka mmoja wa ziada kulingana na muda wa masomo wa ngazi
husika.
i)
Muombaji ataruhusiwa kuahirisha masomo na
kurejea masomoni mwaka unaofuata mara moja tu katika muda wote wa masomo katika
ngazi ya masomo anayopatiwa mkopo. Mkopaji atakayeshindwa kurejea masomoni
mwaka unaofuata baada ya kuahirisha, mkopo wake utasitishwa na kutakiwa kuanza
marejesho ya mkopo.
j)
Muombaji aliyeajiriwa asiwe na madeni kutoka
taasisi nyengine yanayofikia zaidi ya theluthi moja ya mshahara wake kabla na
hadi atakapomaliza mkataba wake wa mkopo na Bodi.